MUSSA MATELEPHONE

MUSSA MATELEPHONE

Monday 1 August 2016

Jinsi ya kuflash simu za kisasa za kichina A.K.A ( Android Smartphones)


Kama kichwa cha post kinavyosema, nataka ujue ni jinsi gani ya kuweza kuflash simu yako ya Android kwa kutumia Proglam mbalimbali kulingana na tatizo binafsi.

Hapa kwanza nitaelezea simu mbalimbali kulingana na aina ya chipset zake


  1.  Tecno= => Infinix= => Gionee= => Innjoo= => Itel= => Elephone= => Jiayu= => Oppson= => THL= => Pipo= => Oppo= => Chuwi, Oppo, Vivo...

    = => Copy za samsung, copy za htc, copy za sony kama (XBO) n.k. hizi chipset zake mara nyingi ni =MTK
  2.    itel, copy za tecno na copy nyingine za samsung, hzo mara nyingi huwa ni SPD  

Matatizo ni kama simu imefikia hatua inawaka haimalizi. kwa maana kama ni tecno inaishia katika logo ya tecno. cha  kufanya ni kuingia hapa  MTK FLASH FILES
 Utadownload mafile kulingana na aina ya simu yako na model yako. ukimaliza itakubid uingie hapa udownload driver hizi hapa Mtk usb flashing drivers
mtkusb driver
Utadownload hii program kwa ajiri ya kuflash ambayo inaitwa  Sp flash tool
kumbuka haya mafile unapoyadownload mengine yatakuwa katika mfumo wa ZIP au RAL kwahyo itakubidi uyaextract kwa kutumia hii proglam  WINRAL. 
 Ukishayaextract andaa simu simu yako kwa kuichaji simu yako hadi 50% at least. fungua folder la sp flash tool humo ndani utakuta mafile mengi ila wewe fungua file linaloitwa flash tool lililopo katika mfumo wa application. angalia kulia katika browser list utaona browse to load scatter file. itafungua window mpya kwa ajiri ya kuselect scatter. hapo utaenda katika folder uliloextract file la simu yako then utachagua mfano kama ni mtk 6572 itakuwa hivi- (MT6572_Android_scatter_emmc) utalifungua hilo na litaload mafile yote unayotakiwa kuyaflash katika simu yako alafu utaclick katika Download. hapo toa betri katika simu subil sekunde kama tatu rudishia bonyeza batani ya kupunguzia sauti na chomeka simu yako katika computer bila kuachilia hyo batani, ukiona msitali mwekundu unapita hadi mwisho achia batani. utapta wa blue alafu utafatia wa njano huo ukimaanisha imeanza kuflash. Hapo tulia uisikilizie hadi imalize. ambapo ikimaliza inaonyesha tick. ukishaona tick chomoa simu yako toa betri na rudshia tena iwashe kawaida.
  • Hapa tena nazungumzia jinsi ya kuziflash hizo za aina ya piri aina ya SPD. Mara nyingi katika kazi zangu nimekutana nazo za aina ya (Itel) hizi Proglam yake ni hii hapa SPD FLASH TOOL 
  • Mafile ya hizo simu yanapatikana hapa SPD FLASH FILES
  • Driver za hzo simu kwa ajiri ya kuflashia ni hizi hapa SPD FLASHING DRIVER
Hizi utatakiwa kuifungua hiyo upgrade tool kutoka katika folder uliloliextract na utaenda katika alama ya kwanza kulia inayoonyesha (load package) utraiclick tena itafungua window itakayokuwa inakutaka ukaload file unalotakiwa kuliflash katika simu yako. kwahyo utatafuta hlo folder ulipoliextract file la simu yako na utaliload katika hyo proglam. likishaingia itakubid uclick katika alama ya kama play itakayokuwa inaonyesha haya maandishi pindi unaposogeza mshale wa mouse yako- (start download) hgapa utatumia njia ile ile ya kushikilia batani ya kushusha au kupandisha sauti  katika kuconnect kama mtk. usisahau kabla ya yote kuinstall driver za simu yako husika. maana bila driver huwezi kufanya lolote.

kwa mara nyingne nitarudi kufundisha jinsi ya kuflash simu za samsung smartphones na Nokia feature kama nokia BB5 na smart kama  NOKIA  LUMIA

Kwa tatizo lolote litakalojitokeza kabla au baada ya kuiflash simu yako niulize  kupitia  namba zangu za simu hizi hapa 0763976109     0658190978  usisahau Kunicheki hapa Facebook.


No comments: